Mjumbe
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa
Viti Maalum Jimbo la Singida, Martha Mlata (kushoto) akisalimiana na
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco)
Dkt. Miganda Manyahi (kulia), jijini Arusha kabla ya kuanza kwa ziara
kwenye miradi ya umeme. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini
inafanya ziara katika miradi ya umeme iliyopo katika mikoa ya Arusha na
Kilimanjaro ili kujionea hatua ya utekelezwaji wake pamoja na kuzungumza
na watendaji.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Richard Ndassa
(kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Daudi Felix Ntibenda
(kulia) mara baada ya Kamati hiyo kuwasili ofisini kwake kwa ajili ya
kupokea taarifa ya mkoa kabla ya kuanza kwa ziara kwenye miradi ya
umeme. Mtaalam
kutoka Kampuni ya Sweco International AB, Pal Aberg (kushoto) akitoa
maelezo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwenye
chumba cha kuendesha mitambo ya umeme ( control room) ndani ya kituo cha
kupooza na kusambaza umeme kilichopo Njiro nje kidogo ya jiji la
Arusha. Meneja
Mradi katika Kituo cha Kupooza na Kusambaza Umeme cha KIA Mhandisi
Emmanuel Manirabona (kulia) akiielezea Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Nishati na Madini hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo hicho kilichopo
mkoani Kilimanjaro.
Post a Comment