tiko
tiko
MAELEZO YA AWALI
Katika maelezo ya awali yaliyotolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabere Marando, ilielezwa kuwa chama hicho kilikuwa kikimfuatilia mlinzi huyo kwa kipindi kirefu baada ya kuhisi kwamba anashirikiana na viongozi wa CCM na maafisa usalama kutaka kukatisha uhai wa Dk. Slaa kwa kumuwekea sumu kwenye chakula au kinywaji.
Katika maelezo ya awali yaliyotolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabere Marando, ilielezwa kuwa chama hicho kilikuwa kikimfuatilia mlinzi huyo kwa kipindi kirefu baada ya kuhisi kwamba anashirikiana na viongozi wa CCM na maafisa usalama kutaka kukatisha uhai wa Dk. Slaa kwa kumuwekea sumu kwenye chakula au kinywaji.
“Kangezi kwa miaka miwili tumebaini
amekuwa akitumika kuvujisha taarifa za Chadema. Amekiri hilo kwa
maandishi na kutaja namba za watu wote wa usalama wa taifa aliokuwa
akiwapelekea taarifa hizo,” alisema Marando na kuendelea kutoa ufafanuzi
wa jinsi mlinzi huyo alivyokuwa akivujisha siri mpaka walipomnasa.
Katika maelezo hayo, Marando alieleza
kuwa wameamua kumfikisha mlinzi huyo polisi kwani alichokuwa anakifanya,
lilikuwa ni kosa la jinai.
KANGEZI AKANUSHA, AIBUA MAPYA
Siku chache baadaye, Kangezi aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Habari Maelezo, Posta jijini Dar es Salaam na kukanusha vikali tuhuma hizo na kuibua mambo mengine mapya.
Akaeleza kwamba hajawahi kuwa na mpango huo isipokuwa yeye ndiye aliyenusurika kifo baada ya kufungiwa chumbani kwa zaidi ya saa sita na viongozi wa chama hicho wakiwa wanamsulubu akiwa uchi wa mnyama.
Siku chache baadaye, Kangezi aliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Habari Maelezo, Posta jijini Dar es Salaam na kukanusha vikali tuhuma hizo na kuibua mambo mengine mapya.
Akaeleza kwamba hajawahi kuwa na mpango huo isipokuwa yeye ndiye aliyenusurika kifo baada ya kufungiwa chumbani kwa zaidi ya saa sita na viongozi wa chama hicho wakiwa wanamsulubu akiwa uchi wa mnyama.
Aliyekuwa mlinzi wa D.r Slaa Khalid Kangezi.
Kangezi alisema alifanyiwa hivyo
akishinikizwa asaini karatasi ya maelezo kuwa ana njama za kutaka kumpa
sumu Dk. Slaa akishirikiana na watu wengine ambapo kutokana na kutishiwa
maisha, alikubali kusaini kwani ndani ya chumba alichokuwa anateswa,
kulikuwa na begi lenye visu ambavyo anadai vilitaka kutumiwa kumuua.
MARANDO AZUNGUMZA NA UWAZI MIZENGWE
Baada ya kupata taarifa juu ya kilichozungumzwa na Kangezi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, Uwazi Mizengwe lilimtafuta tena Marando ambapo alikuwa na haya ya kuzungumza:
“Hilo suala lipo polisi, huyo Kangezi tulimkabidhi kwa polisi kama nilivyosema awali kwa sababu alichokuwa anakifanya lilikuwa ni kosa la jinai.
Baada ya kupata taarifa juu ya kilichozungumzwa na Kangezi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari, Uwazi Mizengwe lilimtafuta tena Marando ambapo alikuwa na haya ya kuzungumza:
“Hilo suala lipo polisi, huyo Kangezi tulimkabidhi kwa polisi kama nilivyosema awali kwa sababu alichokuwa anakifanya lilikuwa ni kosa la jinai.
Kama wao polisi wamemuona hana hatia au
wameshindwa kufanyia upelelezi tulichowaambia, sisi hatuwezi kusema
chochote, hata wakitaka wamuachie ni juu yao.
“Hatuwezi kuendelea kubishana na mlinzi,
sisi tuseme hivi, yeye aseme vile kisha tuendelee kubishana, hatuwezi
kufanya hivyo. Tulichokisema awali ndicho hichohicho, iliyobaki ni kazi
ya polisi,” alisema Marando.
tiko
tiko
Post a Comment