Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

TRAFIKI DAR WAENDESHA ZOEZI LA KUKAMATA BODABODA ZISIZOFUATA SHERIA

tiko tiko
    Askari wa Usalama Barabarani wakiwa wamezikamata baadhi ya pikipiki ambazo madereva wake wamekutwa na makosa mbalimbali eneo la Mbagala Rangi Tatu asubuhi hii, ambapo walilazimika kulipa faini ya shilingi 30,000/=
    Askari wa Usalama Barabarani wakiendelea na ukaguzi wa bodaboda.
            Vijana wakipandisha bodaboda ndani ya gari tayari kwa kuzipeleka Kituo cha Polisi Maturubai kilichopo Mbagala Kizuiani, Dar.
               Askari Polisi wa Usalama Barabarani wakisimamia upandishwaji wa bodaboda hizo kwenye gari tayari kwa kupelekwa kituo cha polisi.
Askari wa Usalama Barabarani wa jijini Dar-es-Salaam wameanzisha msako wa kukamata bodaboda zinazokiuka sheria barabarani kama kutovaa kofia ngumu (helmenti), kupandisha abiria kwa mtindo wa mshikaki, kutokuwa na leseni za udereva na ubovu wa pikipiki hizo, lengo likiwa ni kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na majeruhi.
tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top