Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

ESCROW IMEATHIRI BAJETI, ASEMA WAZIRI WA FEDHA

tiko tiko

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum.
Serikali imesema asilimia tano kati ya 17 inayochangiwa na wahisani wa maendeleo katika bajeti ya mwaka huu imeathirika kutokana na sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum (pichani), alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, baada ya mkutano  kati ya serikali, wadau na wahisani wa maendeleo kwa nchi zinazoendelea.
Lengo la mkutano huo ni kufanya majadiliano ili kufahamu mwenendo mzima wa bajeti ya serikali ulipofikia na maeneo yanayohitaji kurekebishwa.
Mkuya alisema kutokana na sakata la Escrow lililojitokeza baada ya bajeti kupitishwa, wameona ipo haja ya kuangalia upya mfumo mzima na mikakati yao ya utekelezaji wa bajeti hiyo ili kujua kama bado itaendelea kuwa hai katika utekelezaji wake.
“Katika hili tumeona upo umuhimu wa kutazama upya makubalianao na misingi yetu kama imepoteza uhalisia kiutendaji au la ili kujua tutaendeleaje nayo hata baada ya kujitokeza kwa jambo hili,” alisema. 
Aliongeza kuwa kutokana na hatua stahiki na za wazi zilizochukuliwa na serikali, wahisani wameridhika na wataendelea na utekelezaji wa kuchangia bajeti hiyo kama walivyokubaliana.
“Si vyema bajeti ya serikali iathirike kutokana na mambo yanayojitokeza, na hivi sasa fedha tutakazopata tutazielekeza katika maeneo ya barabara, maji na nishati kama ilivyopendekezwa,” alisema.
Alisema wiki mbili kuanzia sasa takribani Dola milioni 44 (zaidi ya Sh. bilioni 50) huku Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika wakijipanga kutoa Dola millioni 227 (Sh. bilioni 409).
Alisema nchi zinazoendelea zinakabiliwa na masharti magumu katika kupewa misaada, hivyo uwapo utaratibu maalum wa upokeaji wa misaada ili kuepusha kukwama pindi  matatizo yanapojitokeza baada ya makubalinao na wahisani. 
Naye Balozi wa Finland nchini, Sinikka Antila, alisema wataendelea kutoa misaada kama walivyoahidi baada ya kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na serikali dhidi ya wote waliohusika katika sakata la Tegeta Escrow. 
“Kutokana na hotuba ya Raisi Kikwete ya Disemba 22, mwaka jana, tumeona jitihada za wazi zilizochukuliwa na Serikali dhidi ya wahusika wa sakata la Escrow, hivyo tutaendelea kuchangia bajeti kama kawaida,” alisema Antila. 
Wahisani wa maendeleo wanaochangia bajeti ni Canada, Denmark, Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Sweden, Uingereza, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Umoja wa Ulaya na Benki ya Dunia.

TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII

tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top