tiko
tiko
Jaji Mkuu, Othman Chande
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande jana aliangua kicheko baada ya
kuulizwa ni lini atatoa tamko la majaji wanaotuhumiwa katika sakata la
Akaunti ya Tegeta Escrow.
Mwishoni
mwa mwaka jana, Bunge liliazimia kwa kuitaka polisi na vyombo vingine
husika vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria
za nchi kwa wote waliotajwa katika taarifa maalumu ya kamati yake ya
Mashirika ya Umma (PAC), kuhusika na vitendo vyote vya kijinai,
kuhusiana na miamala ya Akaunti ya Tegeta Escrow na watu wengine
watakaogundulika kufuatia uchunguzi mbalimbali unaoendelea.
Januari
15, Jaji Chande alikaririwa akisema atalishughulikia mwenye suala
linalohusu majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Profesa Eudes Ruhangisa
na Aloysius Mujulizi, waliotajwa kupata mgawo wa fedha kutoka kwa
aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa IPTL, James Rugemalila.
Hata
hivyo, alipoulizwa jana aliangua kicheko na kubasamu mwishoni na kisha
akasema: “Jamani siwezi kulizungumzia hilo, leo jamani ninazungumzia
maadhimisho ya Siku ya Sheria na Maonyesho ya Wiki ya Sheria.”
Jaji
Chande alisema Mahakama haifanyi uamuzi wa kesi kwa kuangalia hali ya
mtu, lakini akasema ucheleweshwaji wa kesi mbalimbali zikiwamo za
ufisadi wa Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na dawa ya kulevya
unasababishwa na uchunguzi pamoja na mashahidi kutofika mahakamani kwa
wakati pindi wanapohitajika.
Katika
kukabiliana na hali hiyo alisema: “Mahakama imejipanga kikamilifu
kuhakikisha kesi hizo zinasikilizwa mfululizo mwaka huu ili kuondokana
na tatizo la mrundikano wa mashauri ya kesi za muda mrefu.”
Akizungumzia maadhimisho ya Siku ya Sheria, alisema yatafanyika kuanzia kesho hadi Februari 3 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Alisema
maonyesho hayo yanalenga kutoa elimu na huduma za kisheria kwa wananchi
na mgeni rasmi anatarajia kuwa Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi.
Jaji
Chande alisema, katika wiki hiyo itatolewa elimu kuhusu ufunguaji na
uendeshaji mashauri hasa yale yenye ugumu ya mirathi, utatuzi wa mgogoro
kwa njia ya suluhu mwafaka na tozo za Mahakama kulipwa kwa njia ya
benki. Pia, kutakuwapo na matembezi maalumu ya kuadhimisha wiki hiyo
yatakayoongozwa na Mzee Mwinyi na wiki hiyo itahitimishwa na Rais Jakaya
Kikwete.
tiko
tiko
Post a Comment