tiko
tiko

Katika ripoti yake , mdhibiti wa mali ya umma nchini humo,Thuli Madonsela, amesema kuwa Zuma alikiuka sheria za maadili na kujifaidisha na pesa za Umma.
Hata hivyo, ripoti hiyo ilisema kuwa hakudanganya wabunge kuhusu kashfa hiyo. Kadhalika wito umetolewa kuwa Zuma arejeshe sehemu ya pesa hizo ambazo hazikutumika kwa ajili ya usalama wake au vinginevyo.
Vyombo vya habari nchini humo vinadai kuwa baadhi ya pesa za umma zilitumiwa katika kufadhili mahitaji ya kifahari ya bwana Zuma kama bwawa la kuogelea na chumba cha sinema.
Mwandishi wa BBC nchini humo anasema kuwa ripoti hiyo itaathiri pakubwa sifa ya Zuma na chama tawala ANC, huku akijiandaa kwa uchaguzi mkuu katika kipindi cha wiki sita.
SOURCE: BBC
tiko
tiko
Post a Comment