Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

SHOGA, NYUMBA NDOGO UMEZITAKA MWENYEWE

tiko tiko
Jamani hamjambo naona viroho vinawadunda baada ya kuufunua  ukurasa huu na kujiuliza leo kombora linaangukia kwa nani? Jamani narudia sipo kwa ajili ya kuwarusha roho bali mtajirusha wenyewe kutokana na tabia zenu mbaya. Nia yangu ni ile kumuona mwanamke wenzangu mambo ya kike hayampiti kando.
Jamani kuna mambo mengine yanasikitisha, hivi kwa nini umuogope mwanamke mwenzio mwenye viungo kama wewe. Wiki iliyopita nilielezea makosa ya nyuki kukimbia mzinga wake kwa sababu tu mtu katia mkono na kulamba asali yake.
Jamani ukiona mtu katia mkono kwenye mzinga wako ujue asali yako tamu, unatakiwa kuilinda na siyo kuukimbia mzinga ili kuwaruhusu watu wajilambie kwa raha zao, haipendezi. Hizo ni hasira za mkizi na kutoa kafara kwa mvuvi. Nimeliongelea hili kwa vile makavu ya leo yanafanana na hilo.
Juzi nilikutana na mtoto wa shoga yangu akiwa anatoka sokoni, katika mazungumzo yetu si unajua mimi mtu wa utani. Sijui kukasirika kijinga, mtoto wa kike niliumbwa siku Mungu akitabasamu, nami nikawa na umbile la tabasamu siyo wewe uliumbwa Mungu amechoka kila wakati uso kama ndimu, unacheka hujulikani, umenuna hujulikani!
Si kwanza nazungumza wenye sura mbaya bali wenye sura zilizokosa tabasamu, siwezi kumhukumu mtu kwa maumbile kwa vile mimi sijawahi kuumba wangu. Ila nazungumza na tabia za watu, Mungu kawaumba na sura nzuri lakini imeharibika kwa kukunja uso na kupinda midomo!
Hebu tuachane na hayo tuendelee na yetu, basi katika kutaniana si ndiyo aliponieleza kaamua kurudi kwao baada ya mumewe kuoa mwanamke mwingine. Nilimuuliza kipi kikubwa kilichomuondoa kwa mumewe ikiwa dini yake inamruhusu. Alinijibu jibu la kitoto ambalo lipo katika vichwa vya wanawake wengi!
Eti ameondoka kwa vile hawezi kushea mwanaume na mwanamke mwenzake. Jibu lake nililinifanya nimwangalie chini mpaka juu mpaka akashtuka na kuniuliza kulikoni kumuangalia vile.  Nilichomueleza nataka na wewe ukae chini nikueleze uache ujinga!
Jamani ni kweli wanawake tupo kama mdudu wa sikio tusiotaka mshirika, lakini kutokana na hali ya sasa hivi kuwa na wako wa peke yako kazi. Afadhali dini zingine zinaruhusu mpaka wake wanne, lakini dini zilizokataa tunaona jinsi gani viongozi wao wanavyoingia kwenye kashfa ya kuwa na wanawake wengi tofauti na muongozo wao.
Siyo kwamba nahalalisha lakini ukweli ndiyo ulivyo, asilimia kubwa ya nyumba zetu waume zetu wana wanawake zaidi ya mmoja. Wengine tunawakamata na wasichana wetu wa kazi imefikia hata kuwapa ujauzito!
Hii yote inatokana pengine na udhaifu wetu ndani ya ndoa kwani wengi baada ya kuolewa hujisahau na kuamini ukiishaolewa ndiyo kila kitu.Tumekuwa hatuzithamini ndoa zetu kwa kuamini baada ya kuolewa hakuna kingine zaidi kwa mumeo kama umemvulia nguo ya ndani ndiyo baaasi. Tunasahau mwanaume unatakiwa kutunzwa kama mtoto, kwani wewe ndiye kila kitu kwake siyo kasoro zitolewe na mwanamke wa pembeni.
Pengine mumeo hakuwa na wazo la kuongeza mwanamke mwingine, lakini mwanamke mwenzako ameyaona mapungufu yako na kuyafanyia kazi ndiyo yaliyomfanya mumeo aingie kichwakichwa baada ya kunasa, aliendelea kumpa vitu adimu ambavyo kwako hapati. Ili afaidi vizuri anamuoa kabisa ili asile kwa kujificha.
Unaletewa mke mwenza unakimbia kumbe sababu ni wewe. Kaingia ndani hutakiwi kukimbia, jirekebishe, pigana  kuhakikisha unairudisha namba moja yako.

TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII

tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top