Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

KINYAIYA AFUNGUKA MADAI YA KUUZA UNGA

tiko tiko
BAADA ya tetesi kuzagaa kwamba Mtangazaji wa Clouds TV, Benny Kinyaiya anafanya biashara haramu ya kuuza madawa ya kulevya ‘unga’ ambapo husafiri mara kwa mara kinyemela kwenda Ulaya, mwenyewe amefungukia tuhuma hizo.
Mtangazaji wa Clouds TV, Benny Kinyaiya.
Akichati na gazeti hili juzi akiwa nchini Uingereza, Benny alisema kuwa anashangazwa na madai hayo kwani hajawahi na wala hafikirii kufanya biashara hiyo.
“Hizo taarifa ni za uongo kabisa, ni kweli nasafiri mara kwa mara na hata sasa niko Ulaya kwa biashara zangu binafsi lakini hilo la unga siyo kweli, ni uzushi tu. Kuna mambo yangu ya kibiashara nakuja kufanya ambayo siwezi kuyaanika,” alisema Benny.
 
 
 

TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII

tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top