Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

WALIOFANYA UDANGANYIFU KUADHIBIWA, YASEMA NECTA

tiko tiko

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Taifa (Necta) Dk. Charles Msonde.
Hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya waliohusika katika udanganyifu wa mitihani ya kidato cha nne wa mwaka 2014 ambao wanafunzi 184 wamefutiwa matokeo kutokana na udanganyifu huo.
Kati ya wanafunzi waliofutiwa matokeo 128 ni wa kujitegemea kutoka vituo viwili vya P2617 Kisesa mkoani Mwanza na P4806 Ubago Visiwani Zanzibar na 56 ni watahiniwa kutoka shule mbalimbali.
Akitangaza matokeo juzi jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Taifa (Necta) Dk. Charles Msonde, alisema  wameiagiza mamlaka husika kuwachukulia hatua za kinidhamu waliohusika katika vituo hivyo kwa mujibu wa kanuni za utumishi.
“Lazma wahusika wachukuliwe hatua kwani udanganyifu uliojitokeza ni karatasi moja ya kujibia mtihani kuandikwa na watu watatu  tofauti, jambo linaloonyesha  hakukuwa na umakini,” alisema 
Katika matokeo hayo wanafunzi 196,805 (68.33%)  wamefaulu  kati ya watahiniwa wote 288,247 waliofanya mtihani huo huku kiwango cha ufaulu kikipanda  kwa asilimia 10.08  ikilingnishwa  wanafunzi 235,22 wailofaulu  mwaka 2013 (58.25%).
Hata hivyo, kiwango hicho cha ufaulu bado hakijafikia dhamira ya Serikali  ya lengo la Matokeo Makubwa Sasa (BRN) la kufikia aslimia 70,  jambo linalohitaji nguvu zaidi kwa walimu, wanafunzi na wadau wote wa elimu. 
Dk. Msonde alisema matokeo ya mwaka huu yanaonyesha bado ufaulu wa masomo mengi upo chini ya aslimia 50, Hisabati (19.58), Biashara (34.29), Historia (37.41), Jiografia (37.96), Uraia (37.90), Fizikia (46.71) na Kutunza Fedha (42.20).

TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII

tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top