Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

Siasa bila dini ni uendawazimu

tiko tiko


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza katika kikao cha mashauriano cha viongozi wa dini kilichofanyika Febuari mwaka huu. 
Historia ya siasa duniani haitengani kwa kiwango kikubwa na historia ya dini. Vitu hivi viwili kwa maisha ya mwanadamu vimekuwa sambamba na vyenye mafanikio kwa jamii yoyote ile duniani. Kwa upande mwingine dini na siasa vimeleta matatizo makubwa duniani.
Tusipojenga uhusiano mzuri kati ya siasa na dini katika dunia na nchi yetu, tutaendelea kushuhudia machafuko na uharibifu mkubwa wa mali pamoja na mauti dhidi ya binadamu kama yalivyowahi kutokea hapa nchini hasa katika kampeni za kisiasa. Mara nyingi maovu hayo yanasababishwa na uelewa mdogo juu ya uhusiano wa siasa na dini.
Hivi sasa Tanzania imezalisha ugonjwa mpya unaojulikana kwa jina la ‘udini.’ Unapoanza kuingiza udini katika ajira, elimu, afya na siasa ujue kwamba usalama wa nchi upo hatarini.
Kutenganisha kabisa siasa na dini ni kitu kisichowezekana katika dunia ya leo. Ndiyo maana ninaandika kwamba “siasa bila dini ni uendawazimu”.
Uendawazimu
Huwezi kusema wewe unashughulika na siasa halafu ukajidanganya kwamba huhusiki na masuala ya dini, wananchi wengi ni waumini wa madhehebu mbalimbali. Mathalan, Tanzania kuna Waislamu, Wakristo, Wabudha, Wahindu na hata wapagani.
Siasa ambayo haigusi maisha ya waumini inakuwa imejitenga na jamii husika. Kitu muhimu na kinachotakiwa ni kujenga uhusiano mzuri kati ya nyanja hizi mbili bila upotofu.
Katika siasa za Tanzania, nimegundua kwamba kelele za muda mrefu zinazotolewa na Serikali na wanasiasa kuwataka viongozi wa kiroho au wa dini wasichanganye dini na siasa hazina msingi wowote ule kwa vile mambo hayo mawili hayawezikutenganishwa kabisa.
Wanaoshikilia msimamo huo wanaonyesha woga wao juu na uelewa finyu katika masuala ya dini na siasa, hii ni bahati mbaya.
Yesu Kristo hakuhubiri habari za ufalme wa Mungu pekee na kuacha dhambi, bali aligusa masuala ya jamii kama amani, umaskini, kutenda haki, uhusiano mzuri, madhara ya rushwa na ufisadi, wizi wa mali ya umma, utuanzaji wa rasilimali na hata kuponya magonjwa. Na hii ndiyo injili sahihi, yaani injili ya jamii.
Yesu alikuwa akihubiri injili ya jamii, je, sisi sasa hatupaswi kuihubiri injili hiyo? Nini msingi wa hofu ya viongozi wa Serikali na wanasiasa kwa viongozi wa kiroho kuongelea masuala ya kisiasa katika nyumba za ibada?
Kanisa Katoliki lilitoa msimamo wake kuhusiana na kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa; Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Tanzania kupitia kwa Tume ya Haki na Amani kwa ushirikiana na CPT, wametoa waraka au tamko ikipendekeza kusitishwa kwa mchakato wa Kura ya Maoni ili kupisha maandalizi mazuri ya Uchaguzi Mkuu. Je, hapo kanisa limefanya siasa?
-Mwananchi

TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII

tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top