tiko
tiko
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, Shija Ntelezu, ameungana na baadhi ya wana CCM wengine kumuomba Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa, ajitokeze kutangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza
 na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Ntelezu alisema kwa niaba ya
 wana Kishapu wenzake anamuomba Lowassa baada ya kumaliza adhabu 
aliyokuwa akitumikia yeye na wenzake watano ni wakati mwafaka hivi sasa 
wa kutangaza rasmi nia yake kugombea nafasi hiyo ili ampokee kijiti Rais
 Jakaya Kikwete.
Mwenyekiti
 huyo alisema kwa kadri anavyomfahamu Lowassa ni mmoja wa viongozi 
wachapa kazi wazuri hapa nchini na mwenye uwezo wa kutoa maamuzi magumu 
yanapohitajika kutolewa na kwamba ndiye kwa sasa anayeweza kumrithi Rais
 Kikwete na kuendeleza kasi ya kusukuma kasi ya maendeleo 
aliyoyaanzisha.
Alisema
 wakati taifa likielekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu, Oktoba mwaka 
huu ni muhimu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikawa makini kuhakikisha 
kinamteuwa mgombea mwenye uwezo wa kukabiliana na wagombea wengine 
kutoka vyama vya upinzani.
“Sisi
 Kishapu tunaamini iwapo CCM itamsimamisha mgombea jasiri mwenye uzoefu 
wa kiuongozi ambaye pia ana historia nzuri ya uchapaji kazi hapa nchini 
ambaye haitokuwa kazi kubwa kumnadi kwa wapiga kura nafikiri Lowassa 
anatosha kwa nafasi hiyo hivi sasa, yapo mambo mengi makubwa aliyafanya 
wakati wa uongozi wake,”
“Utumishi
 wa Lowassa unafahamika hapa nchini kuanzia ndani ya chama hadi 
Serikalini, kwa sisi wa Shinyanga tunamfahamu zaidi maana aliwahi kuwa 
mtendaji wetu enzi ya TANU, lakini kikubwa tunachokikumbuka ni jinsi 
alivyowezesha kutufanikishia mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa 
Victoria,” alieleza Ntelezu.
Alisema
 ni muhimu vikao mbalimbali vya uteuzi ndani ya CCM vikawa makini katika
 kufikia maamuzi yake na wajumbe wake wasikubali kuyumbishwa na maneno 
ya watu wasiokitakia mema chama hicho na kwamba kimchunguze kwa umakini 
kila mgombea aliyejitokeza bila ya kumpaka sifa mbaya za uongo.
Mwenyekiti
 huyo alifafanua kuwa ushauri wao wa kumtaka Lowassa agombee nafasi hiyo
 ya urais si kwamba wana CCM wengine waliojitokeza hawana sifa hizo, 
bali ni muhimu kumpa kipaumbele mtu mwenye uzoefu mkubwa wa kiutendaji 
ndani ya serikali na chama.
“Ushauri
 wetu usichukuliwe kwamba wana CCM wengine waliokwisha tangaza nia 
hawafai au hawana uwezo na hakuna anayewalaumu, maana ni haki yao ya 
kikatiba, lakini tunaangalia ni yupi miongoni mwao mwenye uwezo zaidi 
atakayeweza kukivusha chama chetu kwa urahisi kwenye uchaguzi mkuu 
ujao,” alieleza.
Akifafanua
 kuhusu uwezo wa Lowassa Ntelezu alitaja baadhi ya mambo makubwa 
aliyoyafanya alipokuwa waziri katika wizara mbalimbali nchini na pale 
alipokuwa waziri mkuu na kutaja baadhi ya shughuli kubwa kuwa ni pamoja 
na maamuzi ya ujenzi wa sekondari za kata ikiwemo ujenzi wa Chuo Kikuu 
cha Dodoma (UDOM).
Lowassa
 pamoja na makada wengine watano, Frederick Sumaye, William Ngeleja, 
January Makamba, Bernard Membe na Stephen Wassira juzi walimaliza rasmi 
kifungo cha miezi 12 walichopewa na kamati kuu ya CCM ikiwa ni adhabu ya
 kukiuka kanuni na taratibu za chama hicho na kuanza kampeni za kuwania 
urais kabla ya wakati.
TOA MAONI YAKO HAPO CHINI KUHUSU HABARI HII
tiko
tiko


Post a Comment