Realtime blog statistics Realtime blog statistics
Scanning..

MKASA BONGOMUVI, SIJUI KESI ITAISHIA WAPI

tiko tiko
Bongomuvi kama kawaida walikuwa wamekodisha nyumba ya pedeshe moja washuti muvi yao. Kazi ikaanza wakagundua kuwa wanahitaji kuweko na mlinzi, basi wakaongea na mlinzi wa kawaida wa nyumba ile na kumwambia kuwa atatokea kwenye muvi na watamlipa, mlinzi akakubali.
Dairekta akampa panga mlinzi na kumwambia, ‘Nikisema eksheni unaanza kumfukuza yule supasta sawa?” Mlinzi akakubali kuwa kaelewa. Ndipo mambo yakaanza, dairekta akaamrisha, ‘Eksheni’  Basi mlinzi akaanza kumfukuza supasta, akamfukuza mpaka supasta alipofika kwenye ukuta, ndipo dairekta alipotoa amri, ‘Cut cut” Mlinzi akaanza kumkata mapanga supasta, mpaka sasa wako hospitali supasta hali yake ni mbaya sana, tunangoja kujua nani atashtakiwa kwa tatizo hili.
tiko tiko

Post a Comment

CodeNirvana
© Haki Zote Zimeifadhiwa Kalamu 1 | designed by tabasamu na ∂αиιєℓι
Code Nirvana
Back To Top