tiko
tiko
Tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Novemba 2012, Abdulrahman Kinana amekuwa na
staili inayonifurahisha sana. Kwa muda mfupi, amekirejesha chama tawala
kule ambako kilistahili kuwa kwa siku zote.
Nilipata fursa ya kukutana naye kwa mahojiano mwanzoni tu mwa uteuzi wake ofisini kwake pale Lumumba. Nilimuuliza maswali mengi kwa kila nilichokuwa na mashaka nacho kuhusu chama chake na nimsifu kwamba niliondoka hapo nikiwa sina chembe ya mashaka.
Nilipata fursa ya kukutana naye kwa mahojiano mwanzoni tu mwa uteuzi wake ofisini kwake pale Lumumba. Nilimuuliza maswali mengi kwa kila nilichokuwa na mashaka nacho kuhusu chama chake na nimsifu kwamba niliondoka hapo nikiwa sina chembe ya mashaka.
Anachokifanya
leo, aliniambia na kunithibitishia kuwa atakifanya. Kukisogeza chama
kwa wahusika, wakulima na wafanyakazi, wanyonge, wanoonewa na
wanaonyimwa haki. Leo tunamuona, akifanya ziara katika mikoa mbalimbali,
lakini siyo tu akikiimarisha chama, bali pia aliwakumbusha viongozi wa
serikali wajibu wao.
Baadhi ya mambo anayoyafanya, sikuwahi
kuyaona yakifanywa na makatibu wakuu wengine wote waliofanya kazi na
Mwenyekiti Jakaya Mrisho Kikwete. Philip Mangula, Yussuf Makamba na
Wilson Mukama, kwangu walikuwa makatibu wakuu wa mazoea, wanachowaza ni
tofauti na walichokifanya, walitimiza majukumu yao ofisini, nje ya hapo
hawahusiki.
Kinana anawafuata siyo tu wanachama,
bali wananchi wote, anawauliza kero zao na kama viongozi wao wanafanya
juhudi zozote kuzitatua. Anawaalika wabunge na viongozi wa serikali
kushiriki mikutano yake na kuwataka kujibu maswali ya wapiga kura wao.
Wengi tumewashuhudia wakiumbuka mbele yake na ilipotokea wakazomewa,
haraka walijihami kuwa wanaowazomea ni wapinzani!
Lakini nimeanza kupata mashaka na ziara
za Katibu Mkuu Kinana. Kwa mbali, ninaona kama zinamjenga zaidi yeye
binafsi kisiasa kuliko matarajio ya wananchi. Hii ni kwa sababu anawajua
viongozi mizigo, wanaozurura na wanaoshinda ofisini, lakini yeye kama
kiongozi mtendaji wa chama, mbona hawachukulii hatua?
Juzi akiwa Singida, aliwaambia wapiga
kura wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kuwa mbunge wao
anashindwa kutatua kero zao kwa sababu anazurura ovyo. Kama Katibu Mkuu
anafahamu udhaifu huu wa waziri wa serikali inayoundwa na chama chake,
nini wajibu wa chama kwa watu kama hawa?
Tatizo letu limeendelea kuwa lilelile, tunajua udhaifu wa watendaji wetu, lakini tunashindwa kuchukua hatua, wepesi wa kusema, waoga wa kuchukua maamuzi, hasa magumu!
Tatizo letu limeendelea kuwa lilelile, tunajua udhaifu wa watendaji wetu, lakini tunashindwa kuchukua hatua, wepesi wa kusema, waoga wa kuchukua maamuzi, hasa magumu!
tiko
tiko

Post a Comment